Logo

    wabunge

    Explore " wabunge" with insightful episodes like "15 FEBRUARI 2024", "Kampeni za wabunge DRC na kero lililojitokeza kwa baadhi ya watu - Desemba 19, 2023", "Kampeni za wabunge DRC na kero lililojitokeza kwa baadhi ya watu - Desemba 19, 2023" and "Kampeni za wabunge DRC na kero lililojitokeza kwa baadhi ya watu - Desemba 19, 2023" from podcasts like ""Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu", "VOA Direct Packages - Voice of America", "Sauti - Voice of America" and "Voice of America"" and more!

    Episodes (4)

    15 FEBRUARI 2024

    15 FEBRUARI 2024
    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Dkt. Tulia Akson, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, IPU ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania anaeleza yaliyojadiliwa katika mkutano wa pamoja kati ya Umoja wa Mabunge Duniani na Umoja wa Mataifa. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na uchambuzi wa neno MBEJAA.Leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani limetoa muongozo mpya na nyenzo za kuboresha usambazaji mdogo wa maji. Mwongozo huo wa “ubora wa maji ya kunywa: usambazaji mdogo wa maji”, na vipengele vinavyohusiana vya ukaguzi wa usafi, unalenga kuboresha ubora wa maji hususan ya kunywa, kujenga utoaji wa huduma thabiti zaidi, na kupambana na kuongezeka kwa magonjwa katika jamii zilizo hatarini na zenye uhaba wa rasilimali hiyo muhimu.Gaza, Leo wakati changamoto ya kukatika kwa umeme ikiendelea katika ukanda huo na kwingineko pia mashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema mashambulizi ya anga yakiendelea kulenga mji wa kusini mwa Gaza wa Rafah na kusambaa kwa ripoti kwamba vikosi vya Israel vimefanya operesheni ya kijeshi ndani ya jengo la hospitali ya Nasser, wasiwasi juu ya uwezekano wa uvamizi wa ardhini wa mji huo wa mpakani wenye wakazi wengi unazidi kuongezeka. Na leo ni siku ya kimataifa ya saratani ya utotoni ambapo mwaka huu shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO linajikita na jukumu muhimu la wazazi, madaktari wa familia na madaktari wa watoto katika kubaini mapema saratani hiyo ya utotoni.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili  leo ukumbi ni wake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “MBEJAA”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
    Logo

    © 2024 Podcastworld. All rights reserved

    Stay up to date

    For any inquiries, please email us at hello@podcastworld.io