Logo

    #iwd

    Explore " #iwd" with insightful episodes like "08 MACHI 2024", "Kuwekeza kwa wanawake ni jawabu sahihi - Guterres" and "The Social Ideas Podcast: #IWD - Give Your Best" from podcasts like ""Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu", "Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu" and "Social Innovation: The Social Ideas Podcast"" and more!

    Episodes (3)

    08 MACHI 2024

    08 MACHI 2024
    Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Flora Nducha anamulika siku ya wanawake duniani kuanzia habari ya kwanza hadi ya mwisho maudhui yakiwa Wekeza kwa wanawake - songesha maendeleo.Katika kusherehekea siku ya wanawake duniani kote Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wanawake na wasichana kwa kupata mafanikio makubwa na kuondoa vikwazo, kuvunja fikra potofu na kuchochea maendeleo kuelekea dunia yenye haki na usawa zaidi.Nchini Afrika Kusini katika jimbo la Western Cape kufuatia mafunzo kuhusu unyanyasaji wa kijinsia yaliyotolewa na kikundi cha wanawake cha Ilitha Labantu kwa vituo kadhaa vya polisi, sasa kuna ushahidi wa wazi kwamba vituo vya polisi vimeweka mazingira rafiki ya kuwasikiliza wanawake walionyanyaswa kuliko ilivyokuwa hapo awali. Anold Kayanda ameufuatilia mradi huo.Makala inatupeleka Kigoma nchini Tanzania kumsikia shuhuda Hadija Alisido ambaye amenufaika na miradi ya FAO.Mashinani tunabisha hodi Mwanza nchini Tanzania kupata maoni kuhusu siku ya wanawake duniani. Karibu!

    Kuwekeza kwa wanawake ni jawabu sahihi - Guterres

    Kuwekeza kwa wanawake ni jawabu sahihi - Guterres
    Katika kusherehekea siku ya wanawake duniani kote Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wanawake na wasichana kwa kupata mafanikio makubwa na kuondoa vikwazo, kuvunja fikra potofu na kuchochea maendeleo kuelekea dunia yenye haki na usawa zaidi.  Leah Mushi na maelezo zaidi.Katika ujumbe wake kwa siku hii Katibu Mkuu Guterres amesema “Pamoja na juhudi wanazozifanya kila siku bado wanakabiliwa na vikwazo vikubwa. Mabilioni ya wanawake na wasichana wanakabiliwa na kuenguliwa, ukosefu wa haki na ubaguzi, ilhali janga lililojikita la ukatili dhidi ya wanawake lilikimomonyoa ubinamu.”Amesema ni vyema kuongeza juhudi ikiwemo za kisheria katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanawake kwani kwa kasi ya sasa itachukua miaka miatatu kupata usawa.Akieleza nini kifanyike amesema “ tunapaswa kuwekeza kwenye miradi ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na kuchochea ujumuishaji wanawake na uongozi wa wanawake kwenye uchumi, teknolojia za kidijitali, ujenzi wa amani na hatua kwa tabianchi.Yote hii inategemea kupatikana kwa fedha kwa ajili ya maendeleo endelevu ili nchi ziwe na fedha za kuwekeza kwa wanawake na wasichana.”Kauli mbiu ya siku ya wanawake kwa mwaka huu ni wekeza kwa wanawake ili kuharakisha maendeleo na Mkuu huyo wa umoja wa Mataifa amesema inatukumbusha kuwa kutokomeza mfumo dume kunahitaji kuweko kwa fedha mezani.“Tunahitaji pia kuongeza idadi ya wanawake viongozi kwenye sekta ya biashara, Benki Kuu na Wizara za Fedha. Hii inaweza kusaidia kuchochea uwekezaji kwenye sera na miradi inayokidhi mahitaji ya wanawake na wasichana.Haki za wanawake zimedhihirisha kuwa njia ya haki ya jamii zenye haki, amani na ustawi. Hii ni vema kwetu sote. “Kwa Pamoja, hebu na tuchukue hatua za haraka kufanya kuwa halisia.”Usawa kwa woteNalo shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN Women linaadhimisha siku hii kwa kufanya mkutano mkubwa katika makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani utakao wakutanisha pamoja viongozi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa masuala ya wanawake. UN Women wamesema katika mwaka huu ambapo karibu nusu ya watu duniani wanaishi katika nchi zinazoshiriki katika uchaguzi, Siku hii ya Kimataifa ya Wanawake ni fursa muhimu ya kufafanua siku zijazo tunazotaka.Wakati mizozo, mabadiliko ya tabianchi na jamii zenye mgawanyiko zikididimiza miongo kadhaa ya maendeleo katika usawa wa kijinsia, UN Women inatoa wito waku "Wekeza kwa wanawake ili Kuharakisha Maendeleo" ili hatimae dunia iweze kufikia faida ya usawa wa kijinsia kwa wote.

    The Social Ideas Podcast: #IWD - Give Your Best

    The Social Ideas Podcast: #IWD - Give Your Best

    In this episode of The Social Ideas Podcast, founder of Give Your Best, Sol Escobar discusses why she created the online clothing donation platform and how it is empowering women from many communities.

    Cambridge Centre for Social Innovation
    Give Your Best

    Follow the Cambridge Centre for Social Innovation on:

    Facebook
    Instagram
    LinkedIn
    Twitter
    YouTube

    Logo

    © 2024 Podcastworld. All rights reserved

    Stay up to date

    For any inquiries, please email us at hello@podcastworld.io